Mangi mmoja shabiki mkubwa wa Liverpool leo amezua balaa asubuhi na mapema. Mangi huyo amejikuta akilala mpaka saa tano asubuhi bila kwenda kazini. Mkewe alijaribu kumwamusha lakini mangi huyo anayefahamika kwa jina la Rafael alimwambia mkewe kwamba leo haendi kazini.
Ilipofika milango ya saa 5 asubuhi bosi wake alimpigia simu kutaka kujua kwa nini hajafika kazini na mazungumzo yao yalikuwa kama ifuatavyo;
Bosi: Hallo Rafael.
Rafael: Hallo bosi.
Bosi: Uko wapi?
Rafael: Nipo nyumbani bosi, kwema?
Bosi: unaniuliza kwema, nikuulize wewe mbona hujaja kazini leo na hujatoa taarifa yeyote?
Rafael: Boasi leo ni siku ya mapumuziko, hujui?
Bosi: Kuna nini?
Rafael: Man U kafungwa na Liverpool jana, hatuendi kazini leo mashabiki wa Liverpool!
Bosi: Huna kazi kuanzia leo bwege wewe! Kawaambie wakuajiri hao Liverpool!
Bosi akakata simu kwa hasira, kilichoendelea sijajua!
**********



