Home Jamii Diamond Aonyesha Utofauti, Amstaafisha Gurumo Kwa Zawadi Ya Gari!

Diamond Aonyesha Utofauti, Amstaafisha Gurumo Kwa Zawadi Ya Gari!

526
0

Kuna msemo unasema asiyekufaa kwa dhiki si rafiki! Inawezekana kweli na pia kuna msemo usemao tenda wema uchape lapa! Misemo hii miwili hufanya maisha ya wanadamu kuwa magumu sana!

Siku za hivi karibuni tumemshuhudia Mzee Gurumo mwimbaji maarufu wa bendi ya Msondo Ngoma akitundika Microfone kwa kuacha kuimba baada ya kuona umri wake sasa haumruhusu. Kwanza ni jambo la kumpongeza sana kwa sababu tumekuwa tukishuhudia wanamuziki wengi wa kundi lake hawafikishi umri alio nao yeye!

TX Moshi, Suleiman Mbwembwe na wengineo ni moja ya wanamsondo ambao naweza kusema wametangulia mbele ya haki wakiwa bado wadogo sana. Hili limekuwa ni pengo la wazi kabisa katika Msondo na hakika kwa sasa Msondo imetetereka kwa sabu imepoteza wapiganaji mhimu sana!

Mzee Gurumo kawahusia mengi wanamuziki chipukizi lakini lililovuta hisia za wengi ni kile kitendo cha msanii Nassib Abdul a.k.a Diamond kumununulia gari mzee Gurumo. Watu wanasema mengi lakini kitendo alichokifanya Diamond ni cha kiungwana na kaheshimu na kutambua thamani ya muziki wa Gurumo!


Wangapi mnachoma CD/DVD za wanamuziki na kucopy na kupaste kwenye Ipad na Computer zenu pasipo kutoa hata shilingi jambo linalowafanya kina Gurumo kuwa ‘maarufu kunuka’? Hii imetokana na baadhi ya maoni ambayo yamekuwa yakitolewa kwenye mitandao ya kijamii yakionyesha wazi kutokuthamini na kutambua kuwa alichokifanya Diamond ni cha kipekee! Sidhani kama amefanya kwa kutaka sifa japo kila binadamu anapenda kusifiwa, kwakuwa Diamond anajulikana sana kila anachokifanya kitajulikana! Kama amejikuta ana ziada ya kumgawia na mwingine iweje iwe ishu sana kwako na hujatoa chochote?

Kwa namna moja au nyingine Diamond kafanya jambo la kiungwana sana na si kwa kutafuta umaarufu kwa sababu hakuna maarufu kama Diamond Tanzania na si kwa kumvunjia heshima mzee Gurumo kwa sababu nina hakika Gurumo anahitaji gari lakini kazi yake haikumlipa kiasi cha kumwezesha anunue gari!

Vunja Mbavu inakusalute Diamond! Umetishia bana!

**********


LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here