Adamu aliamua kwenda safari ya mbali kutafuta maisha baada ya hali ngumu ya kiuchumi. Kabla ya kuondoka, alimvika mkewe chupi ya chuma yenye kufuri imara sana. Ufunguo wa chupi alimwachia rafiki yake wa damu bwana Ngonyani kwa masharti kuwa, kama Adamu hatarudi baada ya miaka minne basi ni ruksa kwa Nyonyani kuifungua ile chupi ili mkewe awe huru kuendelea na maisha yake ya kawaida.
Adamu alianza safari yake na kabla hajafika mbali, alimwona rafiki yake akimkimbilia. Adamu akasimama kumsubiri ali ajue kulikoni! Baada ya kumfikia, Adamu aliuliza,
Adamu: Kulikoni swahiba?
Ngonyani: Umenipa ufunguo usio wenyewe!
**********



