Mlevi mmoja alikuwa ametoka zake baa kalewa ndembendembe anaelekea kwake. Akiwa njiani alifika sehemu moja karibu na shule moja mitaa ya Tandale akaanza kukoja. Si unajua tena ukishabwia chupa zako kadhaa kila kitu wakiona kiko levo!
Akiwa katikati ya shughuli ghafla mlinzi akamwona ikabidi amfate kumwadabisha. Na alipomkaribia mazungumzo yao yalikuwa hivi;
Mlinzi: Unajua hili ni eneo la shule?
Mlevi: Ndiyo najua!
Mlinzi: Kwa nini unakoja hapa?
Mlevi: Kwani pamezuiliwa kukojoa?
Mlinzi: Hicho kibao kimeandikwaje?
Mlevi: USIKOJOE HAPA
Mlinzi: Sasa wewe unafanyaje hapa?
Mlevi:Yesu na Maria, hilo nilijua ni jina la shule!
Mlinzi akachoka!
**********




Mm ningekuwa ndo mlinzi ningemletea noma