Home Vichekesho “Bora Kufa Tu, Maisha Hayana Maana Tena!!”

“Bora Kufa Tu, Maisha Hayana Maana Tena!!”

505
1

Denti mmoja wa chuo fulani hapa kwa JK alijikuta akifanya maamuzi magumu sana ya kujiua mara baada ya kugundua ‘kaumwa na nyuki’ na kuungua kabisa ulimi baada ya kunywa chai bila kuipoza! Denti huyo ambaye alitumia muda na mali zake nyingi kumwinda mrembo mmoja aliyekuwa anasoma naye na ghafla baada ya kula vitu ile roho inapenda akaja kugundua kuwa yule mrembo alikuwa kwenye ‘dozi’!


Uzalendo ukamshinda hivyo akaona hana sababu ya kuishi na aliazimia kujiua kwa sumu ya panya. Kabla ya kutekeleza mpango huo denti huyo aliandika waraka na kueleza sababu za yeye kujiua ili isiwe tabu kutafuta nini kilichosababisha kifo chake.

Huku akiwa anaongea peke yake kwa kuchanganyikiwa, denti huyo alielekea kwenye duka mojawapo na mazungumzo yao yalikuwa hivi,

Denti: Mangi, nigei sumu ya panya maana sioni sababu ya kuishi tena, kaniambukiza! (Huku anatoa noti ya shilingi elfu kumi)

Muuzaji: Hii hapa ndugu!

Denti: Nigei chenji yangu nisepe!

Muuzaji: Sasa chenji ya nini na unaenda kujidunga sumu? Niachie niongeze mtaji bana!

Denti: Wewe Mangi kweli bwege, unaanza kunirithi hata sijafa! Nigei chenji yangu acha kunizingua, unafikiri hela ya sanda watatoa wapi??

**********

1 COMMENT

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here