Bibi Hatari Kwa Kupinga
Bibi mmoja alienda benki, akataka aonane na meneja. Baada ya kusikilizwa alifanikiwa kuonana na meneja kama lilivyokuwa hitaji lake.
MENEJA: Una shida gani bibi?
BIBI: Nataka kufungua akaunti niweke milioni 30 zangu sasa hivi.
MENEJA: Mh! Pesa zote umezipata wapi?
BIBI: Nimezipata kwenye mchezo wa KUPINGA, hata wewe ukitaka tunaweza pinga tu!
MENEJA: Mmh! Tunapingaje?
BIBI: Aah!,rahisi sana, naweka hizi milioni 30 zangu na wewe weka hizo hizo, mpaka kesho saa nne asubuhi
sehemu zako za siri zitayeyuka. Zisipo yeyuka umenila, zikiyeyuka nimekula.
MENEJA: Mmh! Sawa bibi hamna shida..
Basi wakakubaliana kuweka hizo pesa kila mmoja kwa maandishi. Kesho yake asubuhi yule bibi akaenda na mzee
mwingine pale benki. Meneja alivyomuona bibi akasema,
MENEJA: Bibi umeliwa! Sehemu za siri zipo!
BIBI: Sawa sasa mama nitaaminije bila kuzishika?
MENEJA: Njoo tu uhakikishe bibi.
Bibi akaenda na kuanza kumshika yule meneja nyeti zake. Wakati anamshika vile yule mzee aliyekuja naye akawa
ameshika kichwa huku mashozi yakiwa yanamlenga. Meneja akamwuliza bibi
MENEJA: Vipi, mbona yule mzee uliyekuja naye kawa vile?
BIBI: Aah! Yule nilipinga naye kwa milion 90 kuwa naweza kumshika meneja wa benki hii sehemu zake za siri akabisha ndipo nikapinga naye ‘sasa ndio kashaliwa pale anakuna kichwaaaaa!





