Akiongea kwa uchungu na huzuni mbele ya Bimp,Nando ambaye ni Mshiriki wa Tanzania amemlaani mshiriki wa Ghana kwa kumwambukiza GONJWA LA ZINAA… Nando amelinyaka gonjwa la zinaa maarufu kwa jina la “Chlamydia” na hivi sasa yuko katika dozi.Gonjwa hilo amelinasa baada ya kungonoka na SELLY bila KONDOMU…..
Kwa nini Nando hakutumia Kondomu?
Akiongea na Bimp ambaye ni mshiriki toka Ethiopia, Nando amekaririwa akidai kuwa Selly aligoma kutumia kondomu. Kwa kuwa alikuwa na HAMU na tayari stimu zilikuwa juu , Nando anadai kuwa hakuwa na jinsi zaidi ya kulikamua TUNDA bila kulimenya….
Namkariri:
“….You know I hate that bi*ch !
I’m f*cking frustrated cos that bi*ch *Selly* gave me STD! That’s why my blood pressure was high yesterday……!”
“….. Unajua namchukia huyu malaya! Nimepagawa sana kwa ajili yake, Selly kaniambukiza ugonjwa ya zinaa! Ndio maana shinikizo langu la damu lilipanda sana jana…….!”
Kama anachokiongea ni kweli basi inawezekana jumba hili la ‘zinaa’ litaangamiza wengi! Sina hakika kama washiriki wakitaka kuingia mjengoni ni lazima wachunguzwe afya zao ili kujua kama wana magonjwa yanayoambukiza na kama hawafanyiwi vipimo basi huu ni udhaifu mkubwa sana kwa mchezo mchafu kama ule unaoitwa Big Brother Africa ambao kwa upande wangu sioni cha maana wanachokifanya zaidi ya kufanya ngono!
Kuna haja ya Tanzania kuangalia upya uamuzi wa kupeleka washiriki kwani mara zote kila anayeenda huko hutaka akitoka awe maarufu kitu kinachoweza kumpelekea akafanya vioja ili avute akili za watazamaji. Pia kimaadili sidhani kama BBA inataswira chanya kwa watoto wetu. Inawezekana kabisa wapo wanaofurahia kuangalia mchezo huu ila siamini kama una manufaa makubwa kuliko maafa unayoyaleta kwa jamii! Ifikie hatua tusiige kila kitu kinachofanywa na watu ‘weupe’!

