Ni saa saba usiku mwendesha bodaboda mmoja alimalizia kuvuta bangi. Baada ya kumaliza aliingia bafuni na kujimwagia kopo la kwanza na la pili la maji. Ghafla akashtuka na kuanza kupiga makelele na kutoka nje akidai bafuni kuna majini.
Watu wakaja wakamkuta yuko uchi wa mnyama. Wakamwuliza, “kulikoni?”, akasema, “kila akijimwagia maji kichwani nywele hazilowi, lazima bafuni kuna majini”. Walivyomwangalia vizuri kichwani kumbe alikuwa kavaa HELMET. .!!!




