Home Vichekesho Bangi, Bangi, Bangi Nomaaaaaaa!

Bangi, Bangi, Bangi Nomaaaaaaa!

763
0

Ganja

Acheni tu ipigwe marufuku hii bangi maana ina mambo. Kulikuwa na kundi la vijana mateja wavuta bangi waliokuwa wamejificha kwenye pagali moja huku wanavuta bangi zao. Wakati wanaendelea kuvuta kwa bahati mbaya wakaishiwa na kibiriti.

Mateja hao wapatao sita wakaamua kumtuma mmoja wao aende nyumba za karibu na walipokuwa ili akaombe kibiriti. Yule teja aliyechaguliwa akaondoka kwenda kutafuta kibiriti. Kwa kuwa bangi zilikuwa zimekolea, alipozunguka vyumba kadhaa vya jumba hilo bovu alijikuta anatokea kwenye chumba kile kile alichowaacha wale masela wake.

Akawaambia ;

Teja: Oya Masela naomba kibiriti!

Masela: Mwana hata sisi tumeishiwa, tumelituma jembe letu likatuletee, kama vipi kaa hapa usubiri!

CHEZEA BANGI WEYEEEEEEEEEEEE!

**********


LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here