Katika kile kinachosemwa ni kuipa promo Tanzania, ujio wa Rais Obama umeifanya Tanzania iwe midomoni mwa watu wengi sana duniani kwa takribani mwezi mzima uliopita! Hii inaashiria kuwa sasa Tanzania inafahamika vyema duniani.
CNN wameendelea kuipa promo kubwa Tanzania katika kipindi cha Inside AfriCa kilichorushwa jana, CNN imepiga kambi katika mkoa wa Kilimanjaro na hapa wanadadavua uzuri wa mlima Kilimanjaro. Ikumbukwe mlima huu ndo mlima pekee mrefu kuliko yote duniani kwa aina za milima iliyoibuka mmoja mmoja, wanasema milima ya Everest ni mirefu zaidi duniani ndio; lakini zile ni safu za milima, huu ni mlima mmoja ulioinuka zaidi kuliko milima yote duniani na si safu!
Hakika Obama katuletea jambo zuri na la kukumbukwa sana duniani, sidhani kama imewahi kutokea nchi moja ikatembelewa na marais wawili wa Marekani tena wenye kufuatana katika tawala za mihula yao. Kama ipo utaniafahamisha! Sifikirii ujio wa Obama ni wa bure kwa sababu hajanipa pesa au sijamshika mkono kama wengine walivyokuwa wakiota na wakatimiza ndoto zao. Nafikiria jinsi alivyonipa nafasi ya kubuni biashara na kutafuta masoko kirahisi zaidi popote duniani kwa sababu sasa nafahamika zaidi.
Sina hakika kama CNN walipanga kuja na Obama lakini wamefanya kipindi hiki katika muda mwafaka na ni matumaini yangu Tanzania itaendelea kunufaika na utalii kwa wingi mara baada ya ujio wa Obama! Watu wanaweza jiuliza hii nchi ni nchi gani ambayo Obama na Bush wameenda kwa wakati mmoja? Sina hakika sana na dhana iliyopo hapo ila ninachoamini Tanzania sasa inafahamika duniani kote!
Angalia video hii ya kipindi cha INSIDE AFRICA kilichorushwa jana.
Sehemu Ya Kwanza
Sehemu Ya Pili
Sehemu Ya Tatu
Angalia Inside Africa Ya CNN Kuhusu Tanzania Na Mlima Kilimanjaro
