Hili ni moja ya makanisa ya zamani sana duniani lililopo nchini Ethiopia ambalo bado linatumika mpaka leo!
Kuna madhari za kuvutia sana Afrika na huu ndio ukweli, kila unapotembelea nchi mbali mbali za kiafrika kuna vitu utaviona vya kuvutia na kushangaza sana macho na akili. Vitu hivi havipatikani pahala popote duniani. Hivyo Afrika ni hazina kubwa sana ya utalii.
Nchi Ethiopia ni moja ya vivutio vikubwa sana duniani. Ethiopia ni nchi ambayo ina historia kubwa sana. Leo hii utaona majengo ya zamani ambayo yalijengwa karne ya 12 na mpaka leo yanatumika. Shuhudia picha hizi za video, uone maajabu ya Ethiopia.
