Home Vichekesho Kipofu Aua Ili Apate Kuona

Kipofu Aua Ili Apate Kuona

638
0

Mtu mmoja mwenye ulemavu wa macho yaani kipofu alifikishwa mahakamani kwa kosa la kumwuua jirani yake! Baada ya kupandishwa kizimbani na kusomewa mashtaka, jaji alimwuliza mtuhumiwa,

Jaji: Umeshtakiwa kwa kosa la mauaji; je, ni kweli au si kweli?


Mtuhumiwa: Mheshimiwa JAJI, kwa kweli mimi na marehemu tulikuwa na ugomvi. Nilipotaka kumpiga akasema NIUE UONE. Kwa kuwa mimi sijaona tangu nazaliwa na nina hamu sana ya KUONA basi NIKAMWUA. Je, kosa ni la nani?

Jaji akabakia kimyaaaaaaaaaaaaaaaaaaa!

**********