Home Siasa Masikini Balozi Ombeni Sefue Atumbuliwa

Masikini Balozi Ombeni Sefue Atumbuliwa

560
0

Masikini Balozi Ombeni Sefue Atumbuliwa

ombeni

Katika kile kinachotajwa ni tumbua tumbua majipu ya Tingatinga Dr. J.P. Magufuli,  zahama limemwangukia mshika visu na mikasi ya kutumbulia majipu, aliyekuwa Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue.

Saka lake lilianza kama moto wa kifuu pale zilipoanza kuzuka tuhuma juu yake dhidi ya uadilifu wake. Balozi Sefue alijikuta katika wakati mgumu zaidi pale alipohusishwa na uteuzi wa kaimu mkurugenzi mkuu wa NSSF ambaye ni raia wa Uganda, Dr. Carina Wangwe. Dr. Carina Wangwe alidumu katika nafasi yake kwa muda usiozidi saa tano tu kabla ya uteuzi wake kutenguliwa baada ya kubaini makosa ya kikanuni.

Sinema hili lilizidi kunoga pale Balozi Ombeni Sefue aliposema uteuzi wake ulikuwa una makosa kwani Dr. Carina aliteuliwa kuwa mwangalizi tu wa NSSF. Baada ya sinema hii kuonesha kuwa hata mhusika mkuu kafa ndipo prodyuza wa picha hilo alipoingia mchezoni kumaliza sinema.

Huyu Hapa Prodyuza wa Sinema Akimaliza Picha Kwa Upole Kabisa

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here