Hii Soda Ni Dozi Tosha Ya Malaria
Hizi ni biashara za watu lakini lazima tuwe makini. Soda zimekuwa zinatajwa kuwa na changamoto kubwa sana kiafya. Hata matabibu wengi hushauri watu wapunguze au kuacha kabisa matumizi ya soda.
Wakati napitapita mtaani nikaona nipate soda mojo ichangamshe koo. Ndipo nikakutana na soda ambayo ilinishtua kidogo. Soda hii nilikutwa imetengenezwa kwa mchanganyiko wa Kwinini! Je, kwinini hii ndiyo ila ambayo hupatikana katika dozi ya malaria? Mimi hata sijui, kama unajua hili tufahamishe. Kama soda hii ni tiba ya Malaria, tuambizane ili watu tuwe tunajidunga dozi tu!

