Home Vichekesho Mwalimu Mgeni Azua Tafrani

Mwalimu Mgeni Azua Tafrani

605
1

Katika shule moja hivi iliyopo jijini Daslamu, ilifanikiwa kupata mwalimu mpya wa somo la sayansi. Baada ya kuwasili mwalimu huyo alipewa kufundisha darasa la sita. Baada ya kuwasili wwalimu mgeni aliingia darasani kwa mara ya kwanza na kufundisha mfumo wa damu. Katika ufundishaji wake ilimlazimu pia kutumia michoro. Hapo ndipo mwalimu alipoauma kuchora moyo ubaoni ili atoe ufafanuzi mzuri. Kwa vile mwalimu hakuwa hakuwa mchoraji mzuri ule moyo ukaonekana ovyo hovyo tu. Huku akijiamini akauliza wanafunzi,




Malimu: Nimechora nini ubaoni?

Mwanafunzi wa kwanza: Matako.

Mwanafunzi wa pili: Umechora matako mwalimu.

Mwanafunzi wa tatu: Mwalimu hayo ni matakoo kabisa.

Mwalimu kwa hasira akaenda kumwita mwalimu mkuu wa shule kwa madai ya kuwa wanafunzi wamefanya mzaha darasani. Baada ya mwalimu mkuu kuingia darasani akaanza kuhoji,

Mwalimu mkuu wa shule: Kwa nini mnamfanyia mwalimu mzaha?

Wanafunzi:  Hatujafanya mzaha.

Mwalimu mkuu wa shule: Kama hamfanyi mzaha nani kachora matakoo ubaoni?




1 COMMENT

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here