Home Vichekesho Msiba Umeahirishwa

Msiba Umeahirishwa

785
0

jamaa alizowea kila akitaka kulala na hawara yake, alikuwa anamdanganya mke wake anakwenda kulala msibani. Siku moja alidanganya vivyo hivyo mkewe akafunga safari ya kwenda msibani.

Kufika eneo la tukio yule mwanamke hakutokea! Alipojaribu kumtafuta kwa simu akaambiwa wakutane siku nyingine kwani yule mwanamke alipatwa na dharura.


Jamaa ikabidi arudi home. Kufika home mkewe anamwuliza kwa mshangao, “vipi tena mbona umerudi?” Jamaa akajibu haraka haraka, “msiba umeahirishwa hadi siku nyingine!”

**********


LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here