Kwa mara ya kwanza U.S Naval Academy imedhamini ndoa ya jinsia moja kati ya David Bucher (Miaka 49), mhitimu wa muda mrefu wa kituo hicho cha mafunzo anayefanya kazi Pentagon na Bruce Moats (miaka 50) mwenza wake.
Sherehe hizi zilihudhuriwa na wageni waalikwa wapatao 100 huku watoto wa wenza hawa wawili pia wakihudhuria. Aidha msemaji wa kituo hiki, Cmdr. John Schofield alisema,
Harusi hii haikutangazwa sana na si kioja kwa U.S Naval Academy!
Schofield aliongeza,
U.S Naval Academy huandaa viongozi wa baadae na kutangaza utamaduni wa kuheshimu utu wa mtu, nafikiri kwa kufanya ndoa hii ya jinsia moja hapa tumeonyesha dhamira yetu!
Angalia Video Yake Hapa
Chanzo Chetu: NBC News

