Nyumba za kupanga bwana…!
Jamaa alipanga mitaa fulani huko maeneo ya Kindondoni. Kama kawaida ya vijana wakishakuwa na magheto kinachobakia ni kuoa kwa hiyari! Siku ya siku jama huyo alimwopoa demu na akaamua kumleta ghetoni kwake.
Baada ya kumfikisha demu wake shughuli pevu ya ROMANCE ikaanza. Baada ya malavidavi kukolea demu akaanza kuchojoa nguo ili wafanye yao. Kutokana na kunogewa na utamu alivua nguo haraka haraka na ikafika wakati wa kuvua chupi! Demu yule kwa kunogewa alivua mguu mmoja na ule mguu uliobakia akaamu kurusha teke ili chupi ivuke!
Kwa bahati mbaya ile nyumba ilikuwa haina ‘Ceiling board’ hivyo yule demu alivyorusha mguu ili kuvua chupi yake ile chupi ikaruka mpaka chumba kinachofuata na kutua kwenye meza ya baba mwenye nyumba iliyokuwa imepambwa kwa ugali safi na dagaa wa nazi!




