Wantu na ndoa zao; Nafikiri hiki pia ni kioja cha aina yake! Jamaa mmoja siku za hivi karibuni alizua gumzo huko Uganda wakati anafunga ndoa na mpenzi wake! Gumzo hilo lilikuja pale wapenzi hao walipoamua kubadilishana mavazi kama chachandu katika ndoa yao.
Mwanaume alivaa vazi la mwanamke na mwanamke alivaa vazi la mwanaume kama wanavyoonekana pichani. Swali la msingi la kujiuliza ni je, wewe unaweza kufanya hivyo?

