Home Vichekesho Dawa Ya Moto Ni Moto!

Dawa Ya Moto Ni Moto!

1042
3

tax

Kijana mmoja wa kiume alimchukua rafiki yake mmoja wa kike na kutoka naye ‘out’! Kijana huyo alikuwa na gari aina ya Toyota Mark ii. Baada ya kutembelea fukwe za Coco, kijana huyo aliamua kuegesha gari sehemu moja tulivu ili afanye mambo yake!

Kijana huyo alipandisha vioo vya gari kisha akaanza kumdandia demu wake. Baada ya mambo ya chumbani kuendelea kwa muda yule dada aliamua kufunguka.


Msichana: Nilisahau kukwambia mapema, kwa taarifa tu mimi nauza! Kila bao ni Tsh. 20,000/=

Bila hiyana yule kijana akatoa wallet yake na kumkabidhi noti mbili za elfu kumi.

Jua likawa limekimbia sana na yule msichana akawa anataka kurudi kwao ila mpenzi wake alikuwa katulia kwenye usukani huku anasikiliza muziki.  Yule binti ikabidi ahoji,

Msichana: Mbona tumemaliza muda mrefu halafu bado hatuondoki na usiku unaingia?

Kijana wa Kiume: Nilisahau kukwambia mwanzo, mimi ni dereva taxi. Kutoka pale nilipokuchukua mpaka hapa ni Tsh 20,000/=, kukurudisha tena ni tsh. 20,000/=! Nipe 20,000/= utafute usafiri mwingine au nipe 40,000/= nikurudishe nilipokutoa!

**********


3 COMMENTS

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here