Home Video Ipo Siku Tu Atatoka Kwa Staili Hii Hii Ya Kulia

Ipo Siku Tu Atatoka Kwa Staili Hii Hii Ya Kulia

348
0

Steve amekuwa ni kivutio kikubwa sana anaposimama mbele ya Kamera mara zote! Jamaa huyu ni shabiki mkubwa sana wa Yanga na huwa anamwaga machozi timu yake ikifungwa! Amekuwa akitumia usanii wake vizuri wa kulia kujitengenezea jina kiasi kwamba watu wengi japo si wote sasa wanamfahamu Steve!

Kali kuliko zote ni pale alipotaka kushiriki Epiq BSS ya 2012 ili akuze na kuonyesha kipaji chake! Salama Jabir, mmoja wa majaji wa Epiq BSS alimtimua na kumwambia akaishangilie Yanga jambo ambalo lilizua mjadala na kilio kwa Steve! Aliongeaongea maneno ya shombo ila kali kuliko zote ni pale aliposema yeye hana shida ya pesa ila kaja kuonyesha uwezo kuwa ni mwimbaji! Alipoambiwa lini atarekodi nyimbo zake baada ya kukosa nafasi ya Epiq BSS akajibu kwamba hana pesa!


Sasa angekuwa hana shida ya pesa angerekodi kitambo sana nyimbo zake. Lakini kwa sababu hana ndio maana akaja BSS. Ki ukweli jamaa alijichanganya tu nia yake ni kutoka na ninavyoona staili hii ya kulialia itamtoa tu siku moja!

Angalia Video Hii

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here