Home Jamii Watanzania Wakimbilia Biashara Ya ‘Unga’ | Wengi Wanaishia Jela Za Hong Kong,...

Watanzania Wakimbilia Biashara Ya ‘Unga’ | Wengi Wanaishia Jela Za Hong Kong, Vigogo Watajwa!!

692
1

Mkuu Chipukizi ameweka kwenye thread nyingine link yenye habari muhimu na sensitive sana ambazo bado hazijadhibitishwa kuhusiana na biashara ya madawa ya kulevya hapa nchini, lakini naona kama vile haikutiliwa mkazo sana baada ya watu kujikita zaidi kwenye si-hasa. Link hiyo, ina nakala ya barua inayodaiwa kuandikwa Julai 11, 2013 na mfungwa wa Kitanzania kwa niaba ya wafungwa wenzake wa Kitanzania wanaodaiwa kufungwa huko Hong Kong baada ya kukamatwa na madawa ya kulevya.

Kama barua inavyoonyesha, nakala zimetumwa kwa vyombo vya habari vya Tanzania lakini so far bado sijaisoma hii habari ndani ya vyombo vyetu. Labda bado wanaitafiti na kuthibitisha kama ni ya kweli. Ni vigumu kuthibitisha kama yaliyoandikwa kwenye hiyo barua ni ya kweli lakini nadhani labda ingekuwa vizuri kama vyombo vya habari vingejaribu kumwuliza aliyekuwa balozi wetu nchini China, ndugu Phillip Marmo ambaye wafungwa hawa wanadai kwenye barua kuwa alishawahi kuwatembelea huko jela, maana idadi ya wafungwa wa Kitanzania inayodaiwa ni kubwa mno kwa nchi moja.


Habari kwenye link husika inadai kuwa kuna karibu wafungwa 200 wa Kitanzania waliokamatwa na madawa ya kulevya nchini Hong Kong. Kati ya hao 200, tayari 130 wameshakutwa na hatia na wengine 70 wako mahabusu wakisubiri uchunguzi kukamilika. Inadaiwa kuwa kati ya Mei and Juni mwaka huu, Watanzania 50 walikamatwa Hong Hong na China kwa kupatikana na madawa ya kulevya. Kwa kawaida wanaokutwa na hatia nchini Hong Kong, wanafungwa kifungo cha miaka 9 kama wakikubali kosa. Wanaokutwa na madawa ya kulevya lakini wakakataa kosa wanafungwa miaka 21 baada ya kudhibitika mahakamani kuwa walikutwa na hayo madawa.

Kama ni kweli, habari iliyopo kwenye hii barua ya Watanzania walioko jela Hong Kong ni mfano halisi wa kinachotokea sehemu nyingine za dunia, kama Afrika ya Kusini na kwingineko. Inategemewa barua hii itasomwa na watu wengi Afrika, hasa Watanzania na itawafanya wengi waache hata kufikiria kuwa punda wa kubebea madawa ya kulevya. Siyo vibaya kama hii barua itaweza kumfanya hata Mtanzania mmoja tuu anayetumika sasa kama punda wa kubebea madawa ya kulevya kuacha kufanya hivyo. Maana kama yaliyoandikwa kwenye hii ni ya kweli, basi hali ni mbaya tena sana.

Barua yenyewe hiyo hapo chini. Zipo nakala za aina mbili. Nakala ya kwanza ni kwa lugha ya Kiswahili na inadaiwa kuandikwa na mfungwa wa Kitanzania kwa niaba ya wafungwa wengine wa Kitanzania huko Hong Kong. Nakala ya pili imetafsiriwa kwa Kiingereza na anayedaiwa kuwa ni mfungwa mwingine wa Kitanzania huko huko Hong Kong. Waandishi wa barua wametaja mpaka majina ya baadhi ya wahusika wakuu kwenye biashara ya madawa ya kulevya. Kama kweli wanahusika sijui.


Najua kama kawaida threads zinazohusiana na madawa ya kulevya huwa zinakuwa na visitors wengi sana kuliko members. Hii barua inaweza kuwa ya kweli au siyo ya kweli, lakini kama wewe unayeisoma hii thread ni visitor na ni punda wa kubebea madawa ya kulevya ushauri wa bure ni kwamba think once, na siyo twice. Achana kabisa na biashara hii ndugu yangu. Vinginevyo, utaozea jela tena siyo Segerea bali jela za nchi nyingine. Kama unabeba madawa kwenda nchi za China, Singapore, n.k. ukikamatwa adhabu yake ni kifo na hakuna atakayekusadia hapo wakiwemo unaowabebea.

Nakala ya nyaraka hizo kwa kiswahili (PDF)

Nakala ya nyaraka hizo kwa kiingereza (PDF)

Chanzo Chetu

1 COMMENT

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here