Kuna tetesi mjini kwamba kampuni ya kigeni kutoka Sweden iko mbioni kuanzisha kituo cha luninga nchini Tanzania kitakachofahamika kama VIASAT 1, wadukuzi wetu wamebaini. Wakiongea kwa nyakati tofauti maafisa wa juu wa chombo hicho cha habari kipya ambao hawakuwa tayari kutaja majina yao waliieleza VUNJAMBAVU kwamba, “tumeamua kuwekeza Tanzania. Lengo letu ni kuwa kituo bora zaidi Tanzania. Tunajua kuna vituo vingi vya luninga lakini macho yetu yako ITV. Hakuna asiyejua kwamba ITV ndio kituo cha luninga chenye watazamaji wengi zaidi Tanzania. Jukumu letu ni kuonyesha upinzani kwa ITV”, alieleza afisa mmoja wao! “Tumejipanga, tuna vituo vingi duniani na hatukuwahi kufeli na hakika miaka miwili au mitatu ijayo, VIASAT 1 itaongoza tu”, aliongeza afisa huyu.
Aidha huu ni wakati wa IPP kujipanga sana kwani takwimu zinaonyesha EATV inafukuzwa kwa ukaribu zaidi na Clouds TV kutokana na kuwa na soko la aina moja yaani vijana. Hivyo EATV imejikuta ikigawana wateja na Clouds TV kwa kasi kubwa ziaidi. Hatari iliyopo ni kwamba VIASAT 1 wana mtaji mkubwa sana ukilinganisha na ITV hivyo bila shaka jitihada za uhakika zinatakiwa kuhakikisha ITV inawekeza zaidi ili kuendelea kushikilia soko.
Kwa mabadiliko haya makubwa ni dhahiri kwamba vituo vya luninga vinavyofanya kazi kwa mazoea tu na kutuonyesha mataputapu vikaze ‘buti’ kwani viko mbioni kupoteza watazamaji wengi zaidi ya hao vinavyowapoteza kila kukicha kwa habari na vipindi butu!
“Wakati wowote tutaanza kuwa hewani, tunakamilisha mambo mhimu kadha wa kadha ili tuwe hewani. Hiki kituo kitakuwa huru hewani, unaweza kukipata bure kabisa”, alisisitiza afisa mwingine alipododoswa na mdukuzi wetu.
Na Mwandishi Wetu.
**********

mmmmmmmh haya ngoja tutaona.