

Katika kunogesha na kulitia chachandu lile Tamasha la Matumaini ambapo mwaka jana mwanadada, shemeji yetu Wema Binti Sepetu alipeperusha mizuka ya watu mara baada ya kunywea ulingoni pale alipokutana na kifua cha mwanadada mahiri wa Bongo Movie,Jacqueline Wolper na kuonyesha dhahiri alikuwa anapambana na bondia wa uzito wa juu!
Msimu huu mwanadada Wolper amebadilishiwa mpinzani kwani atazichapa na mwanadada nguri, mheshimiwa mbunge wa Kawe kwa tiketi ya CHADEMA BiĀ Halima Mdee!
Mpambano huu unaweza kuvuta hisia za wengi hasa kutokana na umaarufu wa wapambanaji hawa. Kambi zote zimekuwa zikijifua kwa nguvu kuhakikisha siku hiyo mtu anatumbuka nyongo!
Tamasha hili limekuwa likifanyika kila mwaka siku ya Julai 7. Mbali na mpambano huu kutakuwepo burudani kibao!
**********
