Home Jamii Mhabeshi Wa BBA, Betty Huenda Akaenda Jela Miaka 6 Kwa Kufanya Ngono...

Mhabeshi Wa BBA, Betty Huenda Akaenda Jela Miaka 6 Kwa Kufanya Ngono Na Bolt Mjengoni

425
0

Baada ya kutolewa nje ya mjengo wa ‘Kaka Mkubwa Wa Afrika’ yaani Big Brother Africa na kulazimika kuagana na mpenzi wake wa mjengoni Bolt wa Sierra Leone; mrembo Betty Abera kutoka nchini Ethiopia huenda akakabiliwa na kifungo cha mpaka miaka 6 gerezani kwa kosa la kufanya ngono akiwa katika mjengo huo!


Vyanzo mbalimbali vya kwenye mitandao na zikiwemo baadhi ya redio za nchini Ethiopia kama Ethiopikalink, vimeeleza kuwa Betty anaweza kwenda jela kwa miaka 6 iwapo shutuma zinazomkabili zikifanikiwa! kwa kipindi kifupi alichokuwepo BBA, Betty na Bolt walikuwa ni wapenzi wa kwanza kufanya ngono kwa mara ya kwanza ndani ya mjengo msimu huu! Kulikuwa na mashambulizi makali sana kutoka kwa watazamaji zaidi kutoka kwa Wahabeshi ambao kwa sasa wanamwona Betty hana maadili na aliyekosa adabu kwa kuifedhehesha nchi.

Kwa mjibu wa nchi yake, Betty anaweza kukabiliwa na mashitaka ya kufanya ngono hadharani jambo ambalo ni uvunjifu wa sheria za Ethiopia. Lakini jambo la kushangaza ni kwamba, ni kweli Betty anaweza akawa na kesi ya kujibu kwa kitendo hicho? Je, sheria za Ethiopia zinaweza kuvuka mipaka ya nchi mpaka Afrika Kusini kwa Madiba? Kutokana na ukweli kwamba mjengo wa kaka mkubwa wa Afrika umekuwa ukiruhusu ngono za hadharani, je, hawakuliona hilo kabla ya kuruhusu Betty akashiriki? Haya ni mawazo mpingano kiduchu ambayo yanaweza kuibuliwa na wajenga hoja! Unaweza kuchangia chochote kuhusiana na habari hii!

Hii Hapa Video Ya Kutolewa Kwake!!!


LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here