Jamaa mmoja aliamua kumtoa ‘out’ mke wake kwa kumpeleka baa kwa mara ya kwanza kabisa. Haikuwa kawaida yake kwenda baa na mkewe kwani mara zote alikuwa anajumuika na marafiki zake tu.
Wakiwa wanaendelea kupata moja baridi na moja moto akapita binti mmoja ambaye hufanya biashara ya ngono; nina maana ‘changudoa!’ Yule dada changudoa alivyowaona akamsogelea mke wa jamaa na kumnong’oneza,
Changudoa: Shostito, mwambie akulipe chako mapemaaaa kabla hujaondoka naye, jamaa ni mgumu wa kulipa huyu balaaaa!
**********



