Kuna maprofesa arobaini walipanda ndege ya Kitanzania ili wasafari. Kabla ndege haijaanza kuondoka, Lilipita tangazo kama ifuatavyo:
“Ndugu wasafiri wote, ndege unayotarajia kusafiri nayo imetengenezwa na wanafunzi wa Kitanzania na inamilikiwa na shirika la ndege la Tanzania. Tunawatakia safari njema yenye raha mustarehe”
Baada ya tangazo maprofesa wote waliteremka isipokuwa mmoja alibaki kwenye kiti chake anasoma gazeti taratibuuuuu. Walipomuuliza ni kwa nini hakuondoka akajibu kwa haraka na furaha, “kama ndege hii imetengenezwa na watanzania, hata kuwaka haitawaka!”



